Qurani
/
8 - SURAT AL ANFAL/
Aya 2
2- Hakika walioamini kikweli kweli, wakati wote wanaipata hisia ya kumwogopa Mwenyezi Mungu na kumtii. Anapotajwa Mwenyezi Mungu Subhana, basi nyoyo zao huingia woga na kujaa hofu. Na kwa hivyo, kila wanaposomewa aya za Qurani, imani yao inazidi kujikita na wanazidi kumtii na kumjua. Na wala hawamtegemei mwingine yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu Aliyewaumba na ndiye Anayeendelea kuwalinda na kuwastawisha.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map