Qurani
/
7- SURAT AL - ARAAF /
Aya 1
1- Alif, Laam, Miim, Saad. Hizi ni herufi za sauti ambazo hutamkwa mwanzoni mwa baadhi ya sura zilizoteremka Makka kwa ajili ya kuwatanabahisha washirikina kuwa Qurani Takatifu imeundwa kwa herufi zilezile wanazozitamka wao. Na juu ya hivyo, hawawezi kuleta mfano wake. Vilevile, herufi hizi zinaposomwa, huwazindua wao waisikilize Qurani hata ikiwa walikuwa wanashauriana na wakubwa wao kuwa wasiisikilize Qurani.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map