Qurani
/
7- SURAT AL - ARAAF /
Aya 40
40- Hakika wale waliozikadhibisha aya Zetu katika Vitabu na zilizopo ulimwenguni, wakafanya kiburi wasiongoke nazo na wala wasitubie, ni muhali kabisa kwao kukubaliwa vitendo vyao, au kuzipata Rehema za Mwenyezi Mungu au kuingia peponi. Muhali huu ni sawa na uwezekano wa kuingia ngamia kwenye tundu ya sindano! Na kwa mfano huu wa adhabu, Tunawaadhibu wakadhibishaji na wafanyao kiburi katika kila umma.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map