Qurani
/
2- Surat AL - BAQARAH /
Aya 19
19- Au hali yao hiyo ya kubabaika, mambo kuwawia magumu na kutoweza kulitofautisha la kuwadhuru wala la kuwanufaisha, ni kama hali ya watu walionyeshewa na mvua toka mbinguni iliyoambatana na radi na ngurumo kali, wakaweka vidole vyao masikioni wasipate kuzisikia sauti za ngurumo hali ya kuwa wanachelea kufa, wakidhani kwamba kufanya hivyo kutawazuilia na kifo. Wanafiki hawa, inapoteremka Qurani yenye kuwafunulia magiza ya ukafiri na adhabu zake, yenye kubainisha imani na nuru yake inayowaka na yenye kuweka wazi aina mbalimbali za adhabu, wao huipinga na kujaribu kujiweka mbali na hayo wakidhani kwamba kufanya hivyo kutawaondoshea adhabu. Lakini, Mwenyezi Mungu Anawajua vizuri makafiri na Amewadhibiti vyema kwa elimu Yake na uwezo Wake.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map