Qurani
/
2- Surat AL - BAQARAH /
Aya 29
29- Bila shaka, Mwenyezi Mungu ambaye inapasa kumwabudu na kumtii, ndiye Yule Aliyewafanyieni ihsani ya kuwaumbieni neema zote zilizopo ardhini kwa ajili ya faida na manufaa yenu. Kisha, pamoja na kuiumba ardhi na vilivyomo, mapendeleo Yake yameelekea mbinguni kwa kuzifanya mbingu saba zilizopangika. Ndani ya mbingu hizo, kuna mnavyoviona na msivyoviona na Mwenyezi Mungu Anakijua kila kitu vyema.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map