Qurani
/
1-SURAT AL - FAATIHA/
Introduction
(Imeteremka Makka na aya zake 7)Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.Suratul Fatiha Sura hii imeteremka Makka kabla ya hijra. Imeitwa hivyo kwa sababu ndiyo sura ya kwanza katika utaratibu wa Qurani Takatifu. Ni sura ya kwanza iliyoteremka kamili. Inakusanya muhtasari wa Qurani kana kwamba ni kitu cha jumla kinachohitaji kukariri. Makusudio ya Qurani ni: kubainisha tawhidi (kumpwekesha Mwenyezi Mungu), kuonyesha ahadi na habari njema kwa Muumini mwenye vitendo vizuri, kuonyesha onyo na habari mbaya kwa kafiri na afanyaye maovu, kuonyesha ibada, kuonyesha njia ya furaha duniani na akhera na kuvielezea visa vya wale waliomtii Mwenyezi Mungu wakafanikiwa, na visa vya waliomuasi wakashindwa. Na suratul Fatiha, kwa muhtasari na ishara, inakusanya makusudio hayo yote, na kwa hivyo, imeitwa Ummul Kitaab yaani msingi wa Qurani.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map