Qurani
/
11-SURAT HUD/
Aya 1
1- Alif Lam Ra. Hizi ni herufi zilizoanziwa sura hii kwa ajili ya kuashiria kuwa Qurani ni muujiza juu ya kuwa imeundwa kwa herufi hizi hizi wanazozitamka, na kwa ajili ya kuzindua kuisikiliza Qurani Tukufu inaposomwa ya kuwa ni Kitabu chenye shani kuu. Aya zake zimeteremshwa zikiwa zimeshikamana, madhubuti, ndani yake hazina upotovu wala ubabaishi, na zimetungwa kwa njia isiyo na dosari, iwazi, na yenye kubainisha. Kisha hukumu zake zikapambanuliwa. Na Kitabu hichi juu ya utukufu wake chenyewe, kina utukufu zaidi kwa kuwa kimetoka kwa Mwenyezi Mungu Anayekijua kila kitu, na Yeye Subhana Anayaweka mambo katika pahala pake.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map