Qurani
/
14- SURAT IBRAHIM/
Aya 1
1- Alif Lam Ra. Kwa kuanzia kwa herufi hizi, ni kunabihisha muujiza wa Qurani juu ya kuwa imeundwa kwa herufi hizi hizi zinazotumiwa kwa kusemea. Na pia kuwazindua watu waisikilize. Haya yaliyotajwa katika sura hii, ni Kitabu kilichoteremshwa kwako wewe Muhammad kutoka Kwetu, ili uwatoe watu wote toka kwenye giza la ukafiri na ujinga waendee kwenye nuru ya imani na elimu, kwa kusahilishiwa na Mola wao. Na nuru hiyo ndio Njia ya Mwenyezi Mungu Mwenye kushinda kwa kuadhibisha na Mwenye kuhimidiwa kwa kuneemesha.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map