Qurani
/
14- SURAT IBRAHIM/
Aya 4
4- Na Sisi Hatukumtuma Mtume kabla yako, ewe Nabii, ila kwa lugha ya kaumu yake Tuliyomtumia, ili apate kuwafahamisha aliyokuja nayo, nao wayafahamu na wayaelewe kwa wepesi. Wala si juu yake yeye kuwa lazima waongoke. Mwenyezi Mungu Mwenyewe ndiye Humwacha apotee kwa kuwa huyo si tayari kuitaka haki. Na Humwongoa Amtakaye kwa kuwa kajitayarisha vyema kuifuata haki. Na Humwongoa Amtakaye kwa kuwa kajitayarisha vyema kuifuata haki. Naye Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu ambaye Hashindiki kwa Alitakalo, na ambaye Anayapanga mambo mahala pake. Basi Haongoi wala Hapotezi ila kwa hekima.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map