Qurani
/
14- SURAT IBRAHIM/
Aya 9
9- Je, hazijakufikilieni habari za wale waliotangulia kabla yenu? Kaumu ya Nuhu, Adi, Thamudi na umati nyinginezo zilizokuja baada yao ambao hapana anayewajua wingi wao ila Mwenyezi Mungu. Hao walijiwa na Mitume wao kwa hoja zilizowazi ili kuthibitisha ukweli wao. Na hao wakaweka mikono yao kwenye vinywa vyao kwa mastaajabu na kukanya! Wakawaambia Mitume: Sisi kwa yakini tumeikataa miujiza na ishara mlizokuja nazo. Na hakika sisi tuna shaka na hayo mnayotuitia ya kumwamini Mwenyezi Mungu. Sisi hatuyakiniki na chochote, na tuna shaka nayo!
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map