Qurani
/
3- SURAT AL - IMRAN/
Aya 39
39- Hapo Mwenyezi Mungu Alimjibu dua yake. Wakamlingania malaika hali amesimama akielekea kwa Mola wake katika mahala pake pa kufanyia ibada wakimweleza kwamba Mwenyezi Mungu Anakupa habari njema ya kupata mtoto jina lake Yahya atakayemwamini Isa (A.S.) na atakayezaliwa kwa Neno la Mwenyezi Mungu kinyume na wanavyozaliwa watoto wote. Mwenyezi Mungu Atamjaalia (Yahya) kuwa kiongozi kwa watu wake kwa elimu na uchaji, kujiweka mbali na matamanio na kumfanya kuwa kati ya Manabii na watu wema.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map