Qurani
/
3- SURAT AL - IMRAN/
Introduction
(Imeteremka Madina na aya zake 200) Kupitia visa inavyovielezea, Qurani Takatifu inazungumzia juu ya Kanuni za Mwenyezi Mungu katika ulimwengu na mafunzo yanayopatikana. Katika visa hivyo, Qurani Takatifu inayabainisha mengi yanayohusiana na akida, hukumu na mienendo. Katika sura iliyotangulia, Qurani imeelezea sehemu ya sera ya Bani Israili ambapo ndani yake kuna picha nyingi za kukengeuka kwao. Katika sura hii, Qurani inaielezea sehemu nyingine ya upotovu na ukengeukaji wao na inatoa maelekezo juu ya namna ambayo Muumini inabidi awe katika akida yake na mwenendo wake. Aidha, inauweka wazi ukweli wa dini ya mbinguni na kuziashiria adabu za majadiliano. Pia, inaelezea juu ya desturi katika hali ya ushindi na kushindwa. Kadhalika, inabainisha daraja za mashahidi siku ya kiyama, malipo yao watakayolipwa sawa wake kwa waume na njia ya mafanikio. Sura hii, inaanza kwa namna ile ile ilivyoanza sura iliyotangulia.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map