Qurani
/
5- SURAT AL - MAAIDAH /
Aya 1
1- Enyi Waumini! Jilazimisheni kutimiza ahadi zote zilizofanyika kati yenu na Mwenyezi Mungu, na pia ahadi za kisheria zilizofanyika baina yenu na watu wengineo. Na Mwenyezi Mungu Amekuhalalishieni kula nyama za wanyama wa (kufuga) kama ngamia, ngombe, kondoo na mbuzi ila wale mliotajiwa kuwa ni haramu. Wala hamruhusiwi kuwinda barani pale mnapokuwa mmehirimia hija, au mpo katika eneo la (Ardhi Takatifu) Makka. Hakika Mwenyezi Mungu Anahukumu Apendavyo kwa hekima Yake. Na haya ni miongoni mwa Ahadi za Mwenyezi Mungu zilizo juu yenu.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map