Qurani
/
5- SURAT AL - MAAIDAH /
Aya 4
4- Ewe Mtume! Waumini wanakuuliza: Nini Amewahalalishia Mwenyezi Mungu katika vyakula na vinginevyo? Waambie: Mwenyezi Mungu Amekuhalalishieni kila chema kipendacho nafsi njema. Na pia Amekuhalalishieni kula kinachowindwa na wanyama na ndege wakali mliowafunza kuwinda kwa mazoezi kama Alivyokufunzeni Mwenyezi Mungu. Basi kuleni wanachowinda wanyama hao mliowatuma, na msomee Jina la Mwenyezi Mungu pale mnapowapeleka. Na mcheni Mwenyezi Mungu kwa kuzishika sheria Zake na wala msikiuke mipaka Yake. Na tahadharini kuvunja Sheria za Mwenyezi Mungu katika hayo, kwani Yeye ni Mwepesi wa kuhesabu.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map