Main Page

Download
About Islam
Islamic Pillars
Prophetic Tradition
Islamic Encyclopedia
Non-Muslims
Legislation
Creed
Prophet's Stories
Islamic history
Islamic Architecture
Library
Islamic conferences
Islamic conferences
   Qurani /5- SURAT AL - MAAIDAH /
 
Introduction

(Imeteremka Madina na aya zake 120) 

Sura hii ni ya Madina. Idadi ya aya zake ni 120. Sura hii ni kati ya sura za 
Qurani zilizoshuka mwishoni.
Sura hii imekusanya masuala mbalimbali. Miongoni mwa masuala haya 
ni wajibu wa kutimiza maagano kwa ujumla, ni sawa yakiwa baina ya 
mja na Mola wake au baina ya watu wenyewe kwa wenyewe. Kadhalika, 
sura hii imebainisha baadhi ya vyakula vilivyoharamishwa na vilivyo 
halali, na uhalali wa kuwaoa wanawake wa Mayahudi na Wakristo.
Pia sura hii imetaja nguzo za udhu na tayamamu. Kadhalika, imeeleza 
kutakikana kumfanyia uadilifu adui. Vile vile, sura hii imeashiria Neema 
za Mwenyezi Mungu juu ya Waislamu na wajibu wa kukihifadhi Kitabu 
chao. Na ikabainisha kwamba Mayahudi wamebadilisha maneno kutoka 
mahali pake, na Wakristo wamesahau baadhi ya mambo 
waliyokumbushwa na kwamba wao wamekufuru kwa kusema kwao kuwa 
Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu. Kadhalika, sura hii 
inayakanusha madai ya Mayahudi na Wakristo kwamba wao ni wana wa 
Mwenyezi Mungu na vipenzi Vyake. Kisha sura hii imekusanya baadhi 
ya habari za Mayahudi na kisa cha wana wawili wa Adam. Ni kisa 
ambacho kinathibitisha kuwa kufanya uadui ni katika maumbile asili ya 
binadamu. Kisha wajibu wa kuchukua kisasi kwa mwenye kufanya uadui 
kwa ajili ya kuiweka sawa tabia hii mbovu. Vile vile, sura hii imebainisha 
adhabu ya kufanya uasherati na kuiba. Tena baadaye, sura hii ikarejea 
kubainisha ni vipi Mayahudi walivyozipindua hukumu za sheria 
zilizokuwamo katika Taurati, na ikabainisha kwamba katika Taurati na 
Injili, ulikuwepo ukweli na haki kabla ya kugeuzwa geuzwa. Pia sura hii 
imehakikisha kuwa ni lazima kuhukumu kwa mujibu wa Alivyoteremsha 
Mwenyezi Mungu. Hali kadhalika, imeuashiria uadui wa Mayahudi na 
Wakristo wa hivi leo kwa Waumini, na kuwalazimisha Waislamu 
kutowanyenyekea na kutowaridhia kwa wanayowatendea na kuwa ni 
lazima kuwapinga.
Mbali ya hayo, sura imethibitisha ukafiri wa Wakristo waliosema kuwa 
Mwenyezi Mungu ni mmoja wa watatu! Lakini hata hivyo, Qurani 
imewasifu baadhi ya Wakristo walioikubali haki na kuiamini.
Kisha baada ya hapo, sura hii imemkataza Muumini kujiharamishia 
mwenyewe vitu vizuri. Na imebainisha kafara ya kuvunja kiapo. 
Kadhalika, sura hii imeharamisha kabisa ulevi. Na ikabainisha baadhi ya 
vitendo vya ibada ya hija na cheo cha Kaaba na miezi mitakatifu. Kisha 
imebainisha upotovu wa baadhi ya mambo waliyojiharamishia Waarabu 
wenyewe bila ya hoja wala dalili yoyote. Vilevile, sura hii imebainisha 
hukumu ya wasia wakati wa safari.
Mwisho kabisa, sura imehitimishwa kwa kutaja miujiza iliyotokea kwa 
Nabii Isa (A.S), lakini pamoja na miujiza hiyo, Mayahudi walimkanusha. 
Pia sura hii imetaja kuwa Nabii Isa (A.S) hana dhambi ya waliopotoka 
wakamwabudu. Na sura imeeleza Ufalme wa Mwenyezi Mungu Mtukufu 
juu ya mbingu na ardhi na ukamilifu wa uwezo Wake.

        Next


(Imeteremka Madina na aya zake 120) Sura hii ni ya Madina. Idadi ya aya zake ni 120. Sura hii ni kati ya sura za Qurani zilizoshuka mwishoni. Sura hii imekusanya masuala mbalimbali. Miongoni mwa masuala haya ni wajibu wa kutimiza maagano kwa ujumla, ni sawa yakiwa baina ya mja na Mola wake au baina ya watu wenyewe kwa wenyewe. Kadhalika, sura hii imebainisha baadhi ya vyakula vilivyoharamishwa na vilivyo halali, na uhalali wa kuwaoa wanawake wa Mayahudi na Wakristo. Pia sura hii imetaja nguzo za udhu na tayamamu. Kadhalika, imeeleza kutakikana kumfanyia uadilifu adui. Vile vile, sura hii imeashiria Neema za Mwenyezi Mungu juu ya Waislamu na wajibu wa kukihifadhi Kitabu chao. Na ikabainisha kwamba Mayahudi wamebadilisha maneno kutoka mahali pake, na Wakristo wamesahau baadhi ya mambo waliyokumbushwa na kwamba wao wamekufuru kwa kusema kwao kuwa Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu. Kadhalika, sura hii inayakanusha madai ya Mayahudi na Wakristo kwamba wao ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi Vyake. Kisha sura hii imekusanya baadhi ya habari za Mayahudi na kisa cha wana wawili wa Adam. Ni kisa ambacho kinathibitisha kuwa kufanya uadui ni katika maumbile asili ya binadamu. Kisha wajibu wa kuchukua kisasi kwa mwenye kufanya uadui kwa ajili ya kuiweka sawa tabia hii mbovu. Vile vile, sura hii imebainisha adhabu ya kufanya uasherati na kuiba. Tena baadaye, sura hii ikarejea kubainisha ni vipi Mayahudi walivyozipindua hukumu za sheria zilizokuwamo katika Taurati, na ikabainisha kwamba katika Taurati na Injili, ulikuwepo ukweli na haki kabla ya kugeuzwa geuzwa. Pia sura hii imehakikisha kuwa ni lazima kuhukumu kwa mujibu wa Alivyoteremsha Mwenyezi Mungu. Hali kadhalika, imeuashiria uadui wa Mayahudi na Wakristo wa hivi leo kwa Waumini, na kuwalazimisha Waislamu kutowanyenyekea na kutowaridhia kwa wanayowatendea na kuwa ni lazima kuwapinga. Mbali ya hayo, sura imethibitisha ukafiri wa Wakristo waliosema kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja wa watatu! Lakini hata hivyo, Qurani imewasifu baadhi ya Wakristo walioikubali haki na kuiamini. Kisha baada ya hapo, sura hii imemkataza Muumini kujiharamishia mwenyewe vitu vizuri. Na imebainisha kafara ya kuvunja kiapo. Kadhalika, sura hii imeharamisha kabisa ulevi. Na ikabainisha baadhi ya vitendo vya ibada ya hija na cheo cha Kaaba na miezi mitakatifu. Kisha imebainisha upotovu wa baadhi ya mambo waliyojiharamishia Waarabu wenyewe bila ya hoja wala dalili yoyote. Vilevile, sura hii imebainisha hukumu ya wasia wakati wa safari. Mwisho kabisa, sura imehitimishwa kwa kutaja miujiza iliyotokea kwa Nabii Isa (A.S), lakini pamoja na miujiza hiyo, Mayahudi walimkanusha. Pia sura hii imetaja kuwa Nabii Isa (A.S) hana dhambi ya waliopotoka wakamwabudu. Na sura imeeleza Ufalme wa Mwenyezi Mungu Mtukufu juu ya mbingu na ardhi na ukamilifu wa uwezo Wake.

 
Main Page Contact us Links About us Site Map