Qurani
/
16- SURAT ANNAHL /
Aya 39
39- Hakika katika Uadilifu wa Mwenyezi Mungu ni kuwa Atawafufua wote baada ya kufa kwao ili Apate kuwadhihirishia hakika ya mambo waliohitilafiana. Waumini wapate kujua kuwa wao wako katika haki, na makafiri wajue kwamba wao walikuwa makosani kwa kumfanyia Mwenyezi Mungu washiriki katika ungu, na pia ni waongo kwa kuapa kwao kwamba Mwenyezi Mungu Hamfufui anayekufa, na ili makundi yote mawili yapate malipo yao kwa kujua na kwa sababu zake.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map