Qurani
/
13- SURAT AR RAAD/
Aya 1
1- Alif Mym Ra. Herufi hizi ni za kutamkwa zinazoanziwa na baadhi ya sura za Qurani. Nazo zinaashiria kuwa Qurani ni muujiza juu ya kuwa imeundwa kwa herufi wanazozitumia Waarabu katika maneno yao ya kawaida! Na herufi hizi za kutamkwa, zilikuwa zikiwavutia Waarabu waisikilize Qurani. Kwani washirikina waliambizana wasiisikilize Qurani hii. Ikawa Waumini wakianzia herufi hizi za kutamkwa, huvutia masikio ya washirikina wakawa wanaisikiliza. Hakika aya hizo tukufu, ndio hii Qurani; Kitabu chenye shani kubwa, ulichoteremshiwa wewe Nabii kwa haki na ukweli kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Aliyekuumba na Akakuteua. Lakini wengi wa washirikina walioyakanya yaliyokuja ya haki, si watu wa kuikubali haki, bali wao wanaipinga kwa inadi.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map