Qurani
/
13- SURAT AR RAAD/
Aya 4
4- Na hakika ardhi yenyewe ina maajabu! Ndani yake vipo vipande vya ardhi vilivyokaribiana, navyo juu ya hivyo, vina udongo tofauti. Vingine vya ardhi ni yabisi na vingine ni vya rutuba, ijapokuwa ni udongo uleule. Ndani yake, yapo mabustani yaliyojaa miti ya mizabibu, na ndani yake yapo mazao yanayovunwa na mitende inayozaa, nayo ama inakusanyika au iko mbalimbali. Na yote hayo, ijapokuwa inanyweshewa kwa maji yaleyale, lakini yanatofautiana kwa ladha zake. Na hakika katika maajabu haya, zipo dalili wazi za kuonyesha Uwezo wa Mwenyezi Mungu kwa mwenye akili ya kufikiria.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map