Main Page

Download
About Islam
Islamic Pillars
Prophetic Tradition
Islamic Encyclopedia
Non-Muslims
Legislation
Creed
Prophet's Stories
Islamic history
Islamic Architecture
Library
Islamic conferences
Islamic conferences
   Qurani /13- SURAT AR RAAD/
 
Introduction

(Imeteremka Madina na aya zake 43)

Surat “Ar Raad” ni sura ya Madina. Imeitwa “Ar Raad” kwa 
kuzungumzia kwake kwamba radi inamtakasa Mwenyezi Mungu 
Mtukufu. Na idadi ya aya zake ni 43. Imeanza kwa kukibainisha 
cheo cha Qurani Tukufu na kwamba imeteremshwa kwa wahyi 
kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kisha ikaubainisha Ufalme wa 
Mwenyezi Mungu Mtukufu katika ulimwengu na ikazindua kueleza 
mambo yaliyoumbwa kwa uzuri na yenye manufaa ndani yake. 
Kisha ikatoka kuubainisha uwezo Wake Mwenyezi Mungu wa 
kuumba, ikaingia kubainisha uwezo Wake wa kurejesha tena na 
kufufua, na Ujuzi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu wa kila kitu, na 
kuubainisha uwezo Wake wa kuadhibu duniani na kwa hivyo, 
yaweza kukadiriwa kwa adhabu ya akhera. Kisha sura hii 
ikaielekeza miono kuyazingatia maajabu ya ulimwengu ya 
kushangaza. Baada ya hayo, Mwenyezi Mungu Mtukufu Amezielezea 
hali za watu katika kupokea kwao uongofu wa Qurani. Kisha 
Akazitaja sifa za Waumini katika mahusiano yao na ubinadamu, na 
tabia za makafiri na ushupavu wao kushikilia kutaka miujiza 
isiyokuwa Qurani juu ya ubora wake wa cheo, na juu ya kejeli zao 
mbali kabisa dhidi ya Mtume wao. Na Akamweleza Mtume kuwa 
Mitume wa kabla yake pia walifanyiwa kejeli! Pia ni kwamba 
Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye Mwenye kusimamia vitu vyote na 
nafsi zote, na kwamba Yeye ndiye Mwenye kumlipa kila mtu kwa 
anavyostahiki, na kwamba Qurani ndio muujiza mkubwa kabisa 
utakaobaki mpaka siku ya kiyama, na kwamba Mwenyezi Mungu 
Mtukufu ndiye Anayewapa nguvu Mitume Wake kwa miujiza 
Aitakayo. Na ikiwa washirikina wanaukanya utume wa Nabii, basi 
Mwenyezi Mungu Anashuhudia ukweli wake, na Yeye ndiye Mwenye 
kutosheleza kwa hayo.

        Next


(Imeteremka Madina na aya zake 43) Surat “Ar Raad” ni sura ya Madina. Imeitwa “Ar Raad” kwa kuzungumzia kwake kwamba radi inamtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na idadi ya aya zake ni 43. Imeanza kwa kukibainisha cheo cha Qurani Tukufu na kwamba imeteremshwa kwa wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kisha ikaubainisha Ufalme wa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika ulimwengu na ikazindua kueleza mambo yaliyoumbwa kwa uzuri na yenye manufaa ndani yake. Kisha ikatoka kuubainisha uwezo Wake Mwenyezi Mungu wa kuumba, ikaingia kubainisha uwezo Wake wa kurejesha tena na kufufua, na Ujuzi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu wa kila kitu, na kuubainisha uwezo Wake wa kuadhibu duniani na kwa hivyo, yaweza kukadiriwa kwa adhabu ya akhera. Kisha sura hii ikaielekeza miono kuyazingatia maajabu ya ulimwengu ya kushangaza. Baada ya hayo, Mwenyezi Mungu Mtukufu Amezielezea hali za watu katika kupokea kwao uongofu wa Qurani. Kisha Akazitaja sifa za Waumini katika mahusiano yao na ubinadamu, na tabia za makafiri na ushupavu wao kushikilia kutaka miujiza isiyokuwa Qurani juu ya ubora wake wa cheo, na juu ya kejeli zao mbali kabisa dhidi ya Mtume wao. Na Akamweleza Mtume kuwa Mitume wa kabla yake pia walifanyiwa kejeli! Pia ni kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye Mwenye kusimamia vitu vyote na nafsi zote, na kwamba Yeye ndiye Mwenye kumlipa kila mtu kwa anavyostahiki, na kwamba Qurani ndio muujiza mkubwa kabisa utakaobaki mpaka siku ya kiyama, na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye Anayewapa nguvu Mitume Wake kwa miujiza Aitakayo. Na ikiwa washirikina wanaukanya utume wa Nabii, basi Mwenyezi Mungu Anashuhudia ukweli wake, na Yeye ndiye Mwenye kutosheleza kwa hayo.

 
Main Page Contact us Links About us Site Map