Qurani
/
9- SURAT AT TAWBAH/
Aya 40
40- Enyi Waumini! Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi. Hakika Mwenyezi Mungu Anatosha Yeye kumnusuru. Kama pale Alipomnusuru wakati alipotolewa Makka kwa kulazimishwa na makafiri, naye hana mwenziwe isipokuwa Abu Bakr peke yake. Walipokuwa wote wawili katika pango wamejificha wasionekane na washirikina waliokuwa wanawasaka, Abu Bakr akawa anamwogopea Mtume maisha yake. Basi Mtume akamwambia kumtuliza: Usihuzunike! Kwani hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja nasi kwa kutunusuru na kutusaidia. Hapo Mwenyezi Mungu Akamteremshia Abu Bakr utulivu katika moyo wake, na akamunga mkono Mtume kwa majeshi yaliyotoka Kwake ambayo hayajui ila Yeye Mtukufu. Na mambo yakamalizika kwa kujaalia nguvu ya washirikina kuwa dhaifu na Dini ya Mwenyezi Mungu ni yenye kushinda. Na Mwenyezi Mungu Amesifika kuwa ni Mwenye nguvu Hashindwi, na ni Mwenye hekima, mipango Yake haifeli.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map