Qurani
/
10- SURAT YUNUS/
Aya 1
1- Herufi hizi, Mwenyezi Mungu Mtukufu Ameanzia kwazo sura hii. Na Yeye ndiye Anaujua muradi wake. Na juu ya hivyo, zinaashiria kuwa Qurani imeundwa kwa herufi hizi hizi, na nyinyi pamoja na hivyo, mmeshindwa kuleta mfano wake! Na herufi hizi za kutamkwa, zinawazindua washirikina, wakawa wanasikiliza, ijapokuwa wamekubaliana kuwa wasizisikilize aya tukufu hizi na mfano wake ambazo ni aya za Qurani zilizo madhubuti katika mpangilio wake na maana zake, na ambayo imekusanya hekima na kila linalowanufaisha watu katika mambo ya dini na dunia yao.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map