Qurani
/
10- SURAT YUNUS/
Aya 19
19- Watu kwa maumbile yao, hawakuwa ila ni umma mmoja tu kwa mujibu wa umbile la kibinadamu. Kisha Tukawapelekea Mitume wawaongoze na wawaongoe kwa mujibu wa Ufunuo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Tabia hii ya kibinadamu iliyokuwa tayari kwa kheri na shari, imekuwa ndio sababu ya shari kuwa na nguvu zaidi kwa baadhi yao, na kuyafanya matamanio na nyendo za shetani kuwatawala, na kwa hivyo wakahitilafiana. Ewe Nabii! Na lau kuwa hukumu ya Mola wako haikutangulia ya kuwapa muhula makafiri kwa ajili yako na kuyachelewesha maangamizo yao mpaka siku maalumu iliyoahidiwa, basi Mwenyezi Mungu Angaliwapelekea upesi maangamizo na adhabu, kwa sababu ya mfarakano waliyouingia, kama zilivyoingia kaumu zilizokwishapita.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map