Qurani
/
10- SURAT YUNUS/
Aya 3
3- Enyi watu! Hakika Mola wenu ni Mwenyezi Mungu Aliyeumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake katika siku sita ambazo kipimo chake hakijui yeyote ila Mwenyezi Mungu. Kisha Akatandaza utukufu wa ufalme Wake Peke Yake, na Akayapanga mambo yote ya viumbe Vyake. Basi hapana yeyote mwenye chochote pamoja na utawala wa Mwenyezi Mungu na wala hawezi yeyote katika viumbe Vyake kumwombea yeyote isipokuwa kwa ruhusa Yake. Huyo basi, ndiye Mwenyezi Mungu Muumba. Huyo ndiye Mola wenu na ndiye Mlinzi wa neema zenu. Basi mwabuduni Yeye Peke Yake, msadikini Mtume Wake na kiaminini Kitabu Chake. Kwa hiyo ni juu yenu kuzikumbuka Neema za Mwenyezi Mungu na kuzizingatia ishara Zake zinazouthibitisha upweke Wake.
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map