Qurani
/
12- SURAT YUSUF/
Aya 40
40- Hamwabudu badala ya Mwenyezi Mungu ila majina tu mliyoyazua nyinyi na baba zenu kwa dhana bila ya kuwepo ukweli. Mwenyezi Mungu Hakuiteremsha hoja wala ushahidi wa kuwaita miungu. Hapana wa kuhukumu nini kinachofaa kuabudiwa na kipi hakifai ila Mwenyezi Mungu tu. Yeye Ameamrisha msimnyenyekee yeyote mwinginewe, na mumwabudu Yeye Peke Yake. Hiyo ndio dini iliyo nzima na iliyonyooka ambayo ushahidi na dalili zinaelekea kwake. Lakini wengi wa watu hawataki uongozi wa dalili hizi, wala hawajijui kuwa wamo katika ujinga na upotovu!
Main Page
Contact us
Links
About us
Site Map